
Na Mwandishi wetu- Polisi
Madereva wa Serikali katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama wamepatiwa mafunzo maalum ya usalama barabarani yaliyolenga kuongeza uelewa na kuwajengea nidhamu wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.
Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama na kutolewa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Kahama, Mrakibu wa Polisi (SP) Flora Nangawe, ambaye amesisitiza umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu za usalama barabarani ili kupunguza ajali zisizo za lazima.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, SP Nangawe amewataka madereva kuhakikisha hawaendeshi magari wakiwa na leseni zilizokwisha muda wake, akieleza kuwa kufanya hivyo ni kosa la kisheria na linaweza kuhatarisha usalama wa abiria na watumiaji wengine wa barabara.


إرسال تعليق